Katika mji wa St. Mary’s, shule ya Kikatoliki inayosimamiwa na masista wenye bidii ilikumbana na changamoto za kifedha. Masista hawangeweza kuwaomba wazazi waongeze pesa na walimu hawakulipwa kwa wakati. Masisita na walimu walifahamu hali ngumu za wazazi na kwa hiyo, walijadili njia za kupunguza mzigo.
Ili kukabiliana na hali hiyo,
jamii ilipanga kuchangisha pesa. Wafanya-biashara na wazazi walitoa michango
yao. Kwa sababu ya umoja wa watu na kujitolea, shule ilipata matumaini.
Masisita wa Kikatoliki na
jamii walijiunga pamoja kuhakikisha eliu inaaendelea katika shule hiyo. Juhudi
zao za pamoja zilionyesha kwamba, hata wakati hali ni ngumu; walimu, wanafunzi
na jamii, wote wanaweza kuungana na kutatua matatizo ambayo wanapitia.
Kutokana na juhudi za
kuchangisha pesa, shule ya St. Mary’s ilipata mabadikilko mazuri. Walimu
walipokea mishahara hao iliyokuwa imechelewa. Wanafunzi nao walifaidika kwa
kupata vitabu vipya na madarasa bora, wafadhili wakarimu walifurahishwa na matokeo
mazuri ya michango yao.
Barua za shukrani kutoka kwa
wanafunzi na walimu ziliimarisha uhusiano kati ya shule na wafadhili wake. Sasa,
wakati ujaoo wa shule ulionekana kuwa wenye matumaini zaidi kwa sababu ya
juhudi za wote waliohusika.