Friday, 23 February 2024

Ziara ya Zuri

Mwaka uliopita, mwezi wa Septemba, mwanamke mkarimu ambaye anaitwa Zuri pamoja na mvulana wake, walisafiri kutoka Uingereza hadi Kenya. Zuri alinunua mashine mbili za kushona na aliwafundisha wanawake na wasichana jinsi ya kutengeneza pedi au sodo. Zuri alienda kwenye shule ya wasichana na kuwapa wanafunzi vitabu, kalamu na vitu vya kuchorea. Wasichana walifurahi sana na hata waliimba nyimbo za kumshukuru.

Mwanamke mmoja wa Kimaasai alimpa Zuri bangili nzuri na mkufu ambao ulitengenezwa kwa shanga. Wanawake wengine katika kijij hicho pia walimpa zawadi maridadi.

Zuri hakula chakula cha kawaida cha Kimaasai. Badala yake, wanawake wa eneo hilo walitayarisha mandari au kwa jina lingine, pikniki kwa chakula cha mchana. Walileta vitu vitamu kama samosa, chapati, saladi, chai, keki , sandiwichi na matunda. Wote walifurahia sana.

Zuri alikaa Kenya kwa wiki mbili na siku moja akitembelea maeneo tofauti. Hata alifanya kazi na wanawake waliokuwa gerezani. Kando na kushona, pia alishiriki hadithi na kujifunza kutoka kwa wengine.

Zuri hakuishi mahali pake pa kawaida kwa sababu kulikuwa na wageni. Aliishi katika eneo tofauti. Alikaa pamoja na mvulana wake. Ingawa safari ilikuwa ya kuchosha, Zuri na mvulana wake waliifurahia sana.

No comments:

Post a Comment